We capture your memories forever.

Thursday, October 12

MRADI WA UMEME WA MAKAMBAKO-SONGEA KUNUFAISHA MIJI NA VIJIJI 191







NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MAKAMBAKO


KUKAMILIKA kwa Mradi wa ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovolti 220kV, na usambazaji umeme vijijini kutoka Makambako-Songea kupitia Njombe, unatarajiwa kuondoa kabisa tatizo la upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi wa mijini na vijiji vipatavyo 191, Meneja wa Mradi huo Mhandisi Didas Liyamuya,(pichani juu), amesema leo Jumanne Oktoba 10, 2017 wakati wa ziara ya Wahariri wa vyombo vya habari nchini.


Sambamba na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme pia utahusisha upanuzi wa kituo cha kupoza umeme cha Makambako cha msongo wa umeme wa kilovolti 220/132/33Kv, na ujenzi wa vituo vingine vipya viwili, vya Madaba na Songea vya msongo umeme wa kilovolti 220/33kV, halikadhalika ujenzi wa mfumo wa usambazaji umeme wa msongo wa kilovoti 33 pamoja na kuunganisha wateja 22,700, katika mikoa hiyo alisema Mhandisi Liyamuya.


Akifafanua zaidi, katika mkoa wa Njombe, umeme utasambazwa katika maeneo ya Makambako na viunga vyake, Njombe yenyewe, na Ludewa, wakati mkoa wa Ruvuma umeme utasambazwa katika mji wa Songea na vijiji vilivyo katika wilaya ya Mbinga, Namtumbo na Madaba, na kuongeza kuwa umeme utakuwa wa msongo wa kilovolti 33 pamoja na ujenzi wa mawasiliano “OPGW”.


“Lengo la mradi huu ambao unafadhiliwa na Serikali ya Swedena kupitia Shirika lake la Misaada ya Kimaendeleo SIDA, Serikali ya Tanzania na Shirika la Umeme Nchini, TANESCO, ni kuboresha hali ya upatikanaji umeme katika maeneo ya uzalishaji na majumbani.” Alifafanua.


Wahariri hao walipata fursa ya kutembelea eneo la upanuzi wa kituo cha Makambako ambapo walishuhudia kazi ya kujenga misingi ya mitambo ikiwemo Slope protection. Pia walijionea kazi ya kufunga transfoma kwenye maeneo kadhaa ya Makambako ikiwemo eneo la Lyamkena.Mhandisi Liyamuya alibainisha kuwa awamu ya kwanza ya mradi wa kusambaza umeme utakamilika Desemba 2017 wakati awamu ya pili utakamilika Novemba 2018.


“Hadi leo hii Oktoba 10, 2017, mradi umekamilika kwa asilimia 63 kwa upande wa mkoa wa Ruvuma na asilimia 39.5 kwa upande wa mkoa wa Njombe na kazi kubwa iliyofanyika ni ubainishaji wa maeneo ya kupitisha laini (njia ya umeme), ubunifu wa jinsi muundo wa njia hiyo utakavyokuwa, ufyekaji wa njia za kupitisha laini, ununuzi wa vifaa pamoja na kusimamisha nguzo za msongo wa 33kV na 400V na kusambaza nyaya, na usimikaji wa Transofa.” Alisema.


Hata hivyo Mhandisi Lyamuya alieleza masikitiko yake kwa baadhi ya watu kuchoma moto ovyo misitu ambapo baadhi ya nguzo zilizosimikwa katika kipindi hiki cha mradi zimeungua.


“Nitoe rai kwa watanzania wenzangu, Serikali inafanya juhudi kubwa kuwafikishia huduma hii muhimu ya umeme, na mfahamu kwamba fedha za walipa kodi wa Tanzania Shilingi Bilioni 7 zilitolewa kama fidia, iweje leo tuanze kufanya uharibifu huo.?” Alihoji, na kutaka vimgozi wa serikali kwenye maeneo yote ya mradi kuwahamasisha wananchi kutunza miundombinu hiyo ambayo inaligharimu taifa fedha nyingi.

Mmoja wa wakazi wa kitongoji cha Lyamkena, mji wa Makambako mkoani Njombe, ambaye ni mteja mpya wa TANESCO, Bw.Thomas Kiwale, (kulia), akihakikiwa wakati wa zoezi la kuwahakiki wateja walioomba kuunganishiwa umeme kwenye eneo hilo, na afisa wa TANESCO, Bi.Atuokoe Mhingi, Oktoba 10, 2017

Wahariri na mafundi wa TANESCO, wakipita chini ya moja ya transofa zinazoednelea kufungwa kwenye mji wa Makambako Oktoba 10, 2017.

Baadhi ya wahariri wakisikiliza maelzo yaliyokuwa yakitolewa na Mhandisi Liyamuya(hayupo pichani), kuhusu utekeelzaji wa mradi huo walipotembelea eneo la upanuzi wa kituo cha kupoza na kusafirisha umeme wa 220kV cha Makambako.

Baadhi ya wahariri na mafundi wa TANESCO, wakisikiliza maelzo yaliyokuwa yakitolewa na Mhandisi Liyamuya(hayupo pichani), kuhusu utekeelzaji wa mradi huo walipotembelea eneo la upanuzi wa kituo cha kupoza na kusafirisha umeme wa 220kV cha Makambako.
Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bil Leila Muhaji, akifafanua baadhi ya mambo ambapo alisema, ili kujenga uhusiano mwema na wananchi walio jirani na eneo la Mradi, wateja watatozwa kiasi cha shilingi 27,000 tu kwa kazi hiyo katika kipindi hiki cha utekelezaji wa mradi, na hivyo kuwataka wananchi kuwa walinzi wa miundombinu ya umeme kwa faida ya taifa na wao wenyewe.

Bi.Atuokoe Mhingi,kutoka TANESCO, akiendelea na zoezi la kuwahakiki wateja walioomba kuunganishiwa umeme kwenye eneo la Lyamkena, Makambako Oktoka 10, 2017.

Moja ya minara ya kusafirisha umeme wa 220kV. ambao tayari umejengwa nje kidogo ya mji wa Makambako.

Moja ya minara ya kusafirisha umeme wa 220kV. ambao tayari umejengwa nje kidogo ya mji wa Makambako.

Mhariri wa Mwananchi Online Digital, Peter Nyanje, (kushoto) na Mhariri wa gazeti ka Majira, Bw. Mwafisi wakifurahia jambo.





Mhariri wa gazeti la Nipashe, Bw. Joseph Mwendapole, (kulia), akionyeshwa moja ya minara ya kupitisha umeme wa 220kV nje kidogo ya Makambako.
















Kazi ya ujenzi wa msingi wa kufunga mitambo kwenye eneo la upanuzi wa kituo cha kupoza umeme wa 220kV Makambako ikiendelea.







Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji, (kulia) na Afisa Uhusiano wa Shirika hilo, Bi. Grace Kisyombe wakijadiliana jambo.







Meneja Mradi wa ujezni wa njia ya kusafirisha umeme kutoka kampuni ya Isolux,Bw.Elmensour,(kulia), akielezea jinsi kazi hiyo inavyoendelea







Wahariri kutoka kushoto, Peter Nyanje, Joyce Shebe na Nevile Meena

No comments:

Post a Comment