We capture your memories forever.

Showing posts with label Tourism. Show all posts
Showing posts with label Tourism. Show all posts

Saturday, January 6

Zanzibar to Organize a Half Marathon race to Promote Gender Mainstreaming, Attain Sustainable Development Goal



More than 300 Zanzibari women, men, girls and boys are expected to participate in the race ZANZI HALF scheduled to take place on February 4th, 2018 in Stone Town in the Isles.
ZANZI HALF is an international standard sporting and cultural event featuring a half marathon of 10 km and 5 km distances to be staged for the first time in the East African archipelago of Zanzibar with ethe view to highlighting women's empowerment and gender equality.
The race is a response to the 2030 agenda for sustainable development with a call out for action in the world, and is organized by the local interfaith women´s program Upendo Means Love and the Danish NGO and running community Right to Movement in collaboration with ZIFF, Zanzibar International Film Festival (ZIFF) and Zanzibar Amateur Athletic Association (ZAAA).
Women and girls are at the very heart of the agenda in an acknowledgement that their participation is crucial as a pre-condition for the achievement of sustainable development, says one of the organizer,Ms Lotte Bredholt. The race will bring together women and men from the grass root level united in a movement that will translate into further action, transforming gender norms by challenging existing traditional roles, taboo and break down stereotypes showing women and girls as active agents of change and peace. However, sustainability and equality is only achievable if women and men work together.
“Running is empowering” continues Lotte Bredholt, “when women and girls realize their potential and strength on the track and on the streets, there is a spillover effect to other areas of life”. Running is a tool as well for inter-community dialogue continues Lotte Bredholt. Besides the race event, ZANZI HALF encourages local society, rural and urban, to take up running and to be part of a running community. In the meeting between people, sharing experience and passion for a common activity, socio cultural, religious and gender barriers diminish. “It´s a commitment to enhance diversity and inclusion, and is part of the global agenda for sustainable development”.
Fumba Town Development, a project by CPS (FTD),issponsoring the event as part of their support for socio-economic development in Zanzibar. Fumba Town Development combines state-of-the-art residential properties, based on a modern and sustainable infrastructure, with commercial, educational and recreational areas to create a new, modern lifestyle in Zanzibar.
As part of our community development initiatives, we are proud to have teamed up with Zanzihalf for their initial half-marathon on February 4th. We are very excited about the upcoming event and are already training as Fumba Town Team to take part in the race. With regular participants of about 30 runners from our company and the villagers around, we already make an impact towards bringing the communities together.
The Zanzibar Amateur Athletic Association welcomes a race which brings awareness to the role of sport empowering women, however as MlingiBwire points out, a proper half marathon also should have cash prices to attract the elite runners. Though not big, the tree first runners from the two distances 10k and half marathon will be rewarded with a price. All participants will receive a medal.
About the partners
Upendo Women Empowerment is a non-for-profit faith based womens program and social enterprise established in 2005 with the mission of bringing women and girls of different faith together to promote solidarity, trust and peace and to fight poverty by empowering women through vocational training and employment. The vision is a Zanzibar where empowered women and men of different faith contribute to an equal, just and peaceful society, a society where women and men are ready to stand up for human rights, social and economic prosperity and thereby increase equal opportunities in life. In doing so, women and men in Zanzibar become an example of peaceful coexistence and respect between people of different faith.
Right to Movement is a global running community with a growing number of runners, races and communities all over the world running to claim their human right to freedom of movement. RTM is a non-profit, non-religious and non-politic social movement.


Right to Movement came into existence in April 2013, as a conceptual bi-product of the inaugural event Palestine Marathon. Under the slogan “Right to Movement”, RTM held the first ever Palestine Marathon to promote the basic human right to freedom of movement as stipulated under Article 13 in the Human Rights Charter – and to tell a new story about Palestine.


Building on the success of the inaugural Palestine Marathon, Right to Movement establishes running communities and races primarily in countries where the right to free movement is threatened - either for citizens in general or for women in particular. Communities of running activists engaged in the world, with a global and humanitarian outlook who use their love of running to claim their human rights - either for themselves or in solidarity with others. And to inspire others to do the same via their story-sharing on SoMe using the hashtag #righttomovement.In 2016 Right to Movement was awarded as NGO of the year by the organization Sports and Peace in Monaco.


Zanzibar International Film Festival ZIFF also known as Festival of the Dhow Countries is an annual film festival held in Zanzibar. ZIFF is a non-governmental organization established in 1997 and has developed into one of the largest multi-disciplinary art and cultural festival in Africa dedicated to films, music and different form of arts. Over the years, ZIFF has used their platform Women Panorama as a medium of women´s power and visibility to highlight and address pertinent gender and social issues. The Women´s Panorama commonly comprises of a series of workshops, parades, cultural activities, seminars and symposia organized and centered on the visibility of women in and through medium of cinema, the arts and the media.


Registration for the race have started for international and regional participation on the website zanzihalf.com and locally in Stone Town at Upendo Means Love located at Kiponda area, at the heart of the historic stone town. or contact Info@zanzihalf.comt tel +255 (0) 777 120 651. For press contact: Ms. Lotte Bredholt, +255777120561

Wednesday, October 11

VIGUTA WAWAPATIA UZALENDO KWANZA VIWANJA, NYUMBA MKOANI PWANI


Mwenyekiti wa Umoja wa Vicoba Tanzania (Viguta) Taifa, Dk. Dauda Salmin (kulia) akishikana mikono na Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Steve Nyerere mara baada ya kusaini mkataba wa ushirikiano ya kufanyakazi pamoja ambapo UZALENDO KWANZA NA VIGUTA watakuwa bega kwa bega kutoa elimu ya ujasiliamali Tanzania nzima katika hafla iliyofanyika jana Kijiji Cha Kwala - Chalinze. Mwenyekiti wa Umoja wa Vicoba Tanzania (Viguta) Taifa, Dk. Dauda Salmin (kulia) wakisainisha mkataba wa ushirikiano na Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Steve Nyerere ili kuendelea kutoa elimu ya ujasiliamali Tanzania nzima katika hafla iliyofanyika jana Kijiji Cha Kwala - Chalinze.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vicoba Tanzania (Viguta) Taifa, Dk. Dauda Salmin (kulia) akipongezana na Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Steve Nyerere mara baada ya kumaliza kusaini makubaliano.


Salamu za pongezi zikiendelea kutolewa mara baada ya kumaliza zoezi la kusaini mkataba. Mbunge wa viti maalum wa Pwani, Hawa Mchafu Chakoma (CCM) ambaye alikuwa mgeni rasmi akitoa neno kwa wasanii na wananchi walihudhuria hafla hiyo. Mwenyekiti wa Umoja wa Vicoba Tanzania (Viguta) Taifa, Dk. Dauda Salmin akiwatambulisha wanachama


Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Steve Nyerere akitoa neno la shukrani mara baada ya kusaini mkataba wa ushirikino wa kufanya kazi pamoja. Pia aliwashukuru kwa kuweza kuwapatia viwanja kwa ajili ya kujenga nyumba zao za kuishi. Hafla hiyo ilifanyika jana Kijiji Cha Kwala - Chalinze.

Mbunge wa viti maalum wa Pwani, Hawa Mchafu Chakoma (CCM)




Wananchama wa Viguta na Uzalendo Kwanza wafuatilia halfa hiyi.

Wanachama wa Uzalendo Kwanza na Viguta wakielekea eneo la viwanja walivyopewa.

Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Steve Nyerere akikabidhiwa nyumba na Mbunge wa viti maalum wa Pwani, Hawa Mchafu Chakoma (CCM) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika halfa ya ushirikiano na Viguta.


Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza akionyesha mkataba wa nyumba aliyopewa na Viguta.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vicoba Tanzania (Viguta) Taifa, Dk. Dauda Salmin akikabidhiwa nyumba na Mbunge wa viti maalum wa Pwani, Hawa Mchafu Chakoma (CCM) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika halfa ya ushirikiano na Viguta.

Moja ya nyumba aliyopewa mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Steve Nyerere na Viguta.


Burudani ikitolewa.

MAKAMU WA RAIS SAMIA AKUTANA NA MABALOZI WA SAUDI ARABIA, IRELAND NA MOROCCO KWA NYAKATI TOFAUTI DAR ES SALAAM





Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kuzungumza na Balozi wa Ireland nchini Mhe. Paul Sherlock, Ikulu jijini Dar Es Salaam.
Balozi alizungumzia masuala mbalimbali yakiwemo kuwawezesha wanawake katika nafasi za kisiasa, Masuala ya Mimba za utotoni na namna ya kukabiliana na vifo wakati wa kujifungua.
Kwa upande wake Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan aliiomba nchi ya Ireland kuendelea kusaidia Tanzania katika kutoa elimu ya uzazi ili kupunguza Vifo vya akina mama na watoto wakati wa kujifungua.
Wakati huo huo Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amkutana na kuzungumza na Balozi wa Morocco nchini Mhe. Abdelilah Benryane mwenye makazi yake mjini Nairobi,Kenya.
Katika mazungumzo yao, Balozi wa Morocco alimpatia taarifa ya utekelezaji wa yote yaliokubaliwa wakati wa ziara ya Mfalme wa Morocco na kumueleza Makamu kwamba utekelezaji wa mambo hayo umefikia hatua nzuri.
Kwa upande wake Mheshimiwa Makamu wa Rais alimpongeza Balozi kwa kusimamia utekelezaji huo ndani ya muda mfupi.
Makamu wa Rais alimueleza Balozi huyo wa Morocco kuwa uhusiano uliopo kati ya nchi mbili hizi ni wa kudumu na utasaidia katika kukuza uchumi na kuleta maendeleo katika nchi hizi.
Mwisho Kabisa Makamu wa Rais alikutana na kuzungumza na Balozi wa Sausi Arabia Mhe. Mohammed Almalik .


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Saudi Arabia Mhe.Mohammed Almalik(kushoto) aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar Es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Saudi Arabia Mhe.Mohammed Almalik mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar Es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Ireland nchini Mhe. Paul Sherlock alimtembelea Makamu wa Rais ofisini kwake, Ikulu jijini Dar es Salaam.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Morocco Mhe. Abdelilah Benryane (kushoto), Ikulu jijini Dar es salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Morocco Mhe. Abdelilah Benryane (kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo, Ikulu jijini Dar es salaam.

11:Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea taarifa kutoka kwa Balozi wa Morocco Mhe. Abdelilah Benryane (kushoto), Ikulu jijini Dar es salaam. (Picha na Ofisi ya makamu wa Rais)

Wednesday, October 4

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN UZINDUZI WA MAKUMBUSHO MPYA YA OLDUVAI - NGORONGORO




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Makumbusho mapya ya mambo ya kale katika bonde la Olduvai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro, wengine pichani ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Profesa Jumanne Maghembe (kushoto) pamoja na Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (kulia). ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akipiga makofi pamoja na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Profesa Jumanne Maghembe (kushoto) pamoja na Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (kulia) mara baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi wa Makumbusho mapya ya mambo ya kale katika bonde la Olduvai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akipata maelezo mbali mbali kuhusu maisha ya binadamu na wanyama wa kale kutoka kwa Mhifadhi wa Mambo ya Kale kutoka Makumbusho ya Taifa Dkt. Agness Gidna mara baada ya kufungua Makumbusho mapya ya mambo ya kale katika bonde la Olduvai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiangalia historia kuhusu maisha ya binadamu na wanyama wa kale iliyopo kwenye Makumbusho ya Olduvai mara baada ya kufungua Makumbusho mapya ya mambo ya kale katika bonde la Olduvai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.






Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiangalia uzinduzi wa tovuti na mtanzao wa bure wa Hifadhi ya Ngorongoro mara baada ya kufungua Makumbusho mapya ya mambo ya kale katika bonde la Olduvai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.




:Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akihutubia mara baada ya kufungua kufungua Makumbusho mapya ya mambo ya kale katika bonde la Olduvai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Thursday, September 28

WATANZANIA WAMETAKIWA KUENZI UTAMADUNI WETU KUKUZA FURSA ZA UTALII WA KIUTAMADUNI


Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Mbulu


Watanzania wametakiwa kuenzi mila na desturi ambazo ni chanya wazitunze na kuzitumia ili kujenga jamii yenye maadili mema nchini kwa manufaa ya kizazi cha sasa na baadaye.


Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura alipotembelea Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) Haydom wilaya Mbulu mkoani Manyara ambapo amejionea utajiri wa kiutamaduni wenye fursa za utalii wa kiutamaduni.


“Nimetembelea nyumba za asili zilizopo hapa katika kituo hiki nimefurahishwa sana na utajiri wa kiutamaduni uliopo hapa, wazee walizingatia maadili katika kuwalea watoto wao kulingana na mila na desturi zao, ni vema tuenzi utamaduni wetu, huo ni msingi wa maadili mema ya jamii” alisema Naibu Waziri Wambura


Akitolea mfano wa maadili mema yanayopaswa kurithishwa aliyojionea katika kituo cha 4CCP na namna ambavyo watoto waliheshimu nyumba za wazazi wao, Naibu Waziri Wambura amesema kuwa kwa mujibu wa mila na desturi za Kitanzani suala la ulevi na utumiaji wa tumbaku kwa vijana ilikuwa ni mwiko hadi kijana afikie umri wa utu uzima ambapo anaweza kuwa na maamuzi sahihi katika maisha yake yenye kuwa na tija kwa familia.


“Kabla ya kuoa kijana alikuwa haruhusiwi kutumia tumbaku na kunywa pombe, bali kijana akioa na kuwa na watoto wawili kwa mujibu wa mila za makabila ya yaliyopo Mbulu aliruhusiwa kuingia katika kundi la watu wazima na kuruhusiwa kutumia vitu mbalimbali ikiwemo tumbaku na kinywaji cha pombe. Hapa kuna jambo la Watanzania kujifunza na kutunza ili kuondokana na mmomonyoko wa maadili” alisema Naibu Waziri Wambura.


Mila za jamii zilizo njema zinapaswa kutunzwa na kuendelezwa ili ziweze kusaidia vijana na jamii kwa ujumla kuweka mawazo yao katika shughuli za maendeleo pamoja na kupatia familia zao mahitaji ya kila siku.


Naibu Waziri Wambura alisisitiza kuwa mila hizo hazitakiwi kuachwa bali zainatakiwa kuenziwa, kutunzwa, kuendelezwa na kuhifadhiwa kwa manufaa ya sasa ziweze kuchangia katika kukuza utalii wa kiutamaduni ambao ni moja ya vyanzo vya mapato kwa wanajamii na taifa kwa ujumla.


Aidha, Naibu Waziri Wambura alisema kuwa wilaya ya Mbulu ni tajiri katika masuala ya utamaduni na kuongeza kuwa wilaya hiyo ni mdau muhimu katika sekta ya michezo na utamaduni ambazo zinapaswa kuendelezwa kwa manufaa ya taifa.


Kwa upande wake Mbunge wa Mbulu Vijijini Flatei Massay amesema kuwa wilaya hiyo imekuwa na utamaduni wa kufanya tamasha la utamaduni kila mwaka ambapo mwaka huu lilifanyika tarehe 21 hadi 23 mwezi Septemba na inaedelea kuimarisha umoja, mshikamano na ushirikiano miongoni mwa jamii katika masuala mbalimbali ya maendeleo hatua inayopelekea makabila yote kuwa mstari wa mbele katika kudumisha amani ya nchi.


Mbunge huyo aliyataja makabila yanayotokana na makundi makuu manne yanayopatikana wilaya ya Mbulu kuwa ni pamoja na Wairaqw ambao ni jamii ya Wakushi, Wahadzabe jamii ya Khoisan, Wanyiramba na Wanyisanzu jamii ya wabantu na Wadatooga jamii ya Kiniloti.


Naye Mkuu wa wilaya ya Mbulu Chelestino Mofuga amemhakikishia Naibu Waziri Wambura kuwa wilaya hiyo itaendelea kuenzi sekta ya utamaduni kwa kuwa na tamasha la utamaduni linalokutanisha makabila yote wilyani humo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uanuwai wa Utamaduni duniani ambayo hufanyika mwezi Mei tarehe 21 kila mwaka.


Hatua hiyo inatokana na Tanzania kusaini mkataba wa azimio la Umoja wa Mataifa (UN) kuenzi utamaduni na kuheshimu tamaduni za watu wengine chini unaosimamiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).


Mwaka 2002 Umoja wa Mataifa uliamua kuanzisha maadhimisho ya siku ya Utamaduni Duniani kutokana na kuongezeka kwa migogoro, mapigano na kupotea kwa maisha ya watu na mali zao iliyokuwa inatokea sehemu mbalimbali duniani mwishoni mwa miaka ya 1990.



Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (wa pili kushoto) akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Ulinzi na Usalama mara baada ya kuwasili Wilayani Mbulu kwa ziara ya kikazi ya siku mbili wilayani humo.

Mkuu wa wilaya ya Mbulu Chelestino Mofuga akimkaribisha Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura kuongea na wananchi waliokuwa katika tamasha la utamaduni katika Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) Haydom mara baada ya kuwasili Wilayani humo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili wilayani humo.

Baadhi ya Washiriki wa tamasha la utamaduni katika Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) Haydom, wilaya ya Mbullu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (hayupo pichani) alipotembelea kituo hicho.

Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akitoka ndani kujionea moja ya nyumba za asili ya Wabantu Wanyiramba na Wanyisanzu iliyopo Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) kilichopo Haydom.


Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akicheza ngoma na washiriki wa tamasha la utamaduni alipotembelea Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) kilichopo Haydom.

Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (wa pili kulia) akipata maelezo ya utamaduni wa kabila la Wadatoga katika Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) kilichopo Haydom.

Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wasichana wa kabila la Datoga na kusisitiza Watanzania kuenzi utamaduni wetu kwa kuurithisha kwa vijana wetu. Wa nne kushoto ni Mbunge wa Mbulu Vijijini Flatei Massay.(Picha na Eleuteri Mangi, WHUSM, Mbulu)