We capture your memories forever.

Tuesday, July 25

BALOZI MAHIGA APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MABALOZI WATATU








Balozi Mteule wa Jamhuri ya Indonesia




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Jamhuri ya Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Prof. Ratlan Pardede ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo.





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Jamhuri ya Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Prof. Ratlan Pardede. Katika mazungumzo hayo, Mhe. Waziri aliisifu Indonesia kwa hatua ya maendeleo iliyofikia katika nyanja mbalimbali ikiwemo sekta ya kilimo na kuelezea matumaini yake kuwa ujio wa Mhe. Balozi utasaidia kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Indonesia yatakayosaidia Tanzania kujifunza kutokana na maendeleo ya Indonesia.




Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo hayo. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Autralasia, Bi Justa Nyange, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mindi Kasiga na Afisa Dawati, Bw. Emannuel Luangisa






Mwakilishi wa Papa, Tanzania






Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Mwakilishi Mteule wa Papa nchini Tanzania, Mhashamu Marek Solczynski ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo.





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Mteule wa Papa nchini Tanzania, Mhashamu Marek Solczynski.



Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo hayo. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi Mary Matari, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mindi Kasiga na Afisa Dawati, Bw. Ceaser Waitara.





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Mwakilishi Mteule wa Papa nchini Tanzania, Mhashamu Marek Solczynski mara baada ya kuwasili Wizarani kwa ajili ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho.





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akibusu pete ya Mwakilishi Mteule wa Papa nchini Tanzania, Mhashamu Marek Solczynski kabla ya kupokea Nakala za Hati za Utambulisho.





Balozi Mteule wa Ujerumani


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Shirikisho la Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Detlef Wachter ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo.





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule wa Shirikisho la Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Detlef Wachter. Katika mazungumzo hayo, Mhe. Waziri aliishukuru Ujerumani kwa msaada mkubwa inaotoa kwa Tanzania, hususan katika kulinda rasilimali ikiwemo hifadhi za Taifa na kusisitiza umuhimu wa makampuni makubwa ya Kijerumani kuja kuwekeza nchini.





Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo hayo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Itifaki, Bi. Grace Martin, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mindi Kasiga na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi Mary Matari.





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Balozi Mteule wa Shirikisho la Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Detlef Wachter mara baada ya kuwasili Wizarani kwa ajili ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho.




Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment